| ← Titus (2/3) → |
| 1. | Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima; |
| 2. | ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi. |
| 3. | Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; |
| 4. | ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; |
| 5. | na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe. |
| 6. | Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi; |
| 7. | katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, |
| 8. | na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu. |
| 9. | Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu, |
| 10. | wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote. |
| 11. | Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; |
| 12. | nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; |
| 13. | tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; |
| 14. | ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema. |
| 15. | Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote. |
| ← Titus (2/3) → |