| ← Psalms (98/150) → |
| 1. | Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. |
| 2. | Bwana ameufunua wokovu wake, Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake. |
| 3. | Amezikumbuka rehema zake, Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. Miisho yote ya dunia imeuona Wokovu wa Mungu wetu. |
| 4. | Mshangilieni Bwana, nchi yote, Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. |
| 5. | Mwimbieni Bwana zaburi kwa kinubi, Kwa kinubi na sauti ya zaburi. |
| 6. | Kwa panda na sauti ya baragumu. Shangilieni mbele za Mfalme, Bwana. |
| 7. | Bahari na ivume na vyote viijazavyo, Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake. |
| 8. | Mito na ipige makofi, Milima na iimbe pamoja kwa furaha. |
| 9. | Mbele za Bwana; Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa adili. |
| ← Psalms (98/150) → |