| ← Psalms (87/150) → |
| 1. | Msingi wake upo Juu ya milima mitakatifu. |
| 2. | Bwana ayapenda malango ya Sayuni Kuliko maskani zote za Yakobo. |
| 3. | Umetajwa kwa mambo matukufu, Ee Mji wa Mungu. |
| 4. | Nitataja Rahabu na Babeli Miongoni mwao wanaonijua. Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi; Huyu alizaliwa humo. |
| 5. | Naam, mintarafu Sayuni itasemwa, Huyu na huyu alizaliwa humo. Na Yeye Aliye juu Ataufanya imara. |
| 6. | Bwana atahesabu, awaandikapo mataifa, Huyu alizaliwa humo. |
| 7. | Waimbao na wachezao na waseme, Visima vyangu vyote vimo mwako. |
| ← Psalms (87/150) → |