| ← Psalms (70/150) → |
| 1. | Ee Mungu, uniokoe, Ee Bwana, unisaidie hima. |
| 2. | Waaibike, wafedheheke, Wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu. |
| 3. | Warudi nyuma, na iwe aibu yao, Wanaosema, Ewe! Ewe! |
| 4. | Washangilie, wakufurahie, Wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako Waseme daima, Atukuzwe Mungu. |
| 5. | Nami ni maskini na mhitaji, Ee Mungu, unijilie kwa haraka. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Bwana, usikawie. |
| ← Psalms (70/150) → |