| ← Psalms (54/150) → | 
| 1. | Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe, Na kwa uweza wako unifanyie hukumu. | 
| 2. | Ee Mungu, uyasikie maombi yangu, Uyasikilize maneno ya kinywa changu. | 
| 3. | Kwa maana wageni wamenishambulia; Watu watishao wananitafuta nafsi yangu; Hawakumweka Mungu mbele yao. | 
| 4. | Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia; Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu. | 
| 5. | Atawarudishia adui zangu ubaya wao; Uwaangamize kwa uaminifu wako. | 
| 6. | Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu; Ee Bwana, nitalishukuru jina lako, maana ni jema. | 
| 7. | Kwa kuwa limeniokoa na kila taabu; Na jicho langu limeridhika Kwa kuwatazama adui zangu. | 
| ← Psalms (54/150) → |