| ← Psalms (4/150) → |
| 1. | Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Umenifanyizia nafasi wakati wa shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu. |
| 2. | Enyi wanadamu, hata lini utukufu wangu utafedheheka? Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo? |
| 3. | Bali jueni ya kuwa Bwana amejiteulia mtauwa; Bwana atasikia nimwitapo. |
| 4. | Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. |
| 5. | Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini Bwana. |
| 6. | Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mema? Bwana, utuinulie nuru ya uso wako. |
| 7. | Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai. |
| 8. | Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama. |
| ← Psalms (4/150) → |