| ← Psalms (30/150) → |
| 1. | Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu. |
| 2. | Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya. |
| 3. | Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni. |
| 4. | Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake. |
| 5. | Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha. |
| 6. | Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele. |
| 7. | Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika. |
| 8. | Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua. |
| 9. | Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako? |
| 10. | Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu. |
| 11. | Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha. |
| 12. | Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele. |
| ← Psalms (30/150) → |