| ← Psalms (150/150) |
| 1. | Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake. |
| 2. | Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake. |
| 3. | Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi; |
| 4. | Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi; |
| 5. | Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana. |
| 6. | Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya. |
| ← Psalms (150/150) |