← Psalms (149/150) → |
1. | Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa. |
2. | Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya, Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao. |
3. | Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie. |
4. | Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu. |
5. | Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao. |
6. | Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao. |
7. | Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya kabila za watu. |
8. | Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma. |
9. | Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya. |
← Psalms (149/150) → |