← Psalms (147/150) → |
1. | Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri. |
2. | Bwana ndiye aijengaye Yerusalemu, Huwakusanya waliotawanyika wa Israeli. |
3. | Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao. |
4. | Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina. |
5. | Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka. |
6. | Bwana huwategemeza wenye upole, Huwaangusha chini wenye jeuri. |
7. | Mwimbieni Bwana kwa kushukuru, Mwimbieni Mungu wetu kwa kinubi. |
8. | Huzifunika mbingu kwa mawingu, Huitengenezea nchi mvua, Na kuyameesha majani milimani. |
9. | Humpa mnyama chakula chake, Wana-kunguru waliao. |
10. | Hapendezwi na nguvu za farasi, Wala hairidhii miguu ya mtu. |
11. | Bwana huwaridhia wao wamchao, Na kuzitarajia fadhili zake. |
12. | Msifu Bwana, Ee Yerusalemu; Msifu Mungu wako, Ee Sayuni. |
13. | Maana ameyakaza mapingo ya malango yako, Amewabariki wanao ndani yako. |
14. | Ndiye afanyaye amani mipakani mwako, Akushibishaye kwa unono wa ngano. |
15. | Huipeleka amri yake juu ya nchi, Neno lake lapiga mbio sana. |
16. | Ndiye atoaye theluji kama sufu, Huimwaga barafu yake kama majivu, |
17. | Hutupa mvua ya mawe kama makombo, Mbele ya baridi yake ni nani awezaye kusimama? |
18. | Hulituma neno lake na kuviyeyusha, Huuvumisha upepo wake, maji yakatiririka. |
19. | Humhubiri Yakobo neno lake, Na Israeli amri zake na hukumu zake. |
20. | Hakulitendea taifa lo lote mambo kama hayo, Wala hukumu zake hawakuzijua. Haleluya. |
← Psalms (147/150) → |