← Psalms (143/150) → |
1. | Ee Bwana, uisikie sala yangu, uzisikilize dua zangu, Kwa uaminifu wako unijibu kwa haki yako. |
2. | Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki. |
3. | Maana adui ameifuatia nafsi yangu, Ameutupa chini uzima wangu. Amenikalisha mahali penye giza, Kama watu waliokufa zamani. |
4. | Na roho yangu imezimia ndani yangu, Moyo wangu ndani yangu umesituka. |
5. | Nimezikumbuka siku za kale, Nimeyatafakari matendo yako yote, Naziwaza kazi za mikono yako. |
6. | Nakunyoshea mikono yangu; Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame. |
7. | Ee Bwana, unijibu hima, roho yangu imelegea; Usinifiche uso wako, Nisifanane nao washukao shimoni |
8. | Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi, Kwa maana nimekutumaini Wewe. Unijulishe njia nitakayoiendea, Kwa maana nakuinulia nafsi yangu. |
9. | Ee Bwana, uniponye na adui zangu; Nimekukimbilia Wewe, unifiche. |
10. | Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa, |
11. | Ee Bwana, unihuishe kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni; |
12. | Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu; Na kuwaangamiza wote wanitesao nafsi, Kwa maana mimi ni mtumishi wako. |
← Psalms (143/150) → |