← Psalms (141/150) → |
1. | Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo. |
2. | Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni. |
3. | Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu. |
4. | Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa. |
5. | Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; Kichwa changu kisikatae, Maana siachi kusali kati ya mabaya yao. |
6. | Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge, Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu. |
7. | Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu. |
8. | Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana, Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu. |
9. | Unilinde na mtego walionitegea, Na matanzi yao watendao maovu. |
10. | Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, Pindi mimi ninapopita salama. |
← Psalms (141/150) → |