← Psalms (140/150) → |
1. | Ee Bwana, uniokoe na mtu mbaya, Unihifadhi na mtu wa jeuri. |
2. | Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huondokesha vita. |
3. | Wamenoa ndimi zao kama nyoka, Sumu ya fira i chini ya midomo yao. |
4. | Ee Bwana, unilinde na mikono ya mtu asiye haki; Unihifadhi na mtu wa jeuri; Waliowaza kuzipotosha hatua zangu. |
5. | Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba; Wametandika wavu kando ya njia; Wameniwekea matanzi. |
6. | Nimemwambia Bwana, Ndiwe Mungu wangu; Ee Bwana, uisikie sauti ya dua zangu. |
7. | Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita. |
8. | Ee Bwana, usimpe asiye haki tamaa zake, Usiifanikishe hila yake, wasije wakajiinua. |
9. | Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, Madhara ya midomo yao yawafunike. |
10. | Makaa ya moto yawaangukie, watupwe motoni, Na katika mashimo, wasipate kusimama tena. |
11. | Msingiziaji hatawekwa imara katika nchi, Mtu wa jeuri, uovu humwinda kumwangamiza. |
12. | Najua ya kuwa Bwana atamfanyia mnyonge hukumu, Na wahitaji haki yao. |
13. | Hakika wenye haki watalishukuru jina lako, Wenye adili watakaa mahali ulipo Wewe. |
← Psalms (140/150) → |