← Psalms (139/150) → |
1. | Ee Bwana, umenichunguza na kunijua. |
2. | Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; Umelifahamu wazo langu tokea mbali. |
3. | Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote. |
4. | Maana hamna neno ulimini mwangu Usilolijua kabisa, Bwana. |
5. | Umenizingira nyuma na mbele, Ukaniwekea mkono wako. |
6. | Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, Hayadirikiki, siwezi kuyafikia. |
7. | Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako? |
8. | Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. |
9. | Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; |
10. | Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika. |
11. | Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; |
12. | Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa. |
13. | Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu. |
14. | Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana, |
15. | Mifupa yangu haikusitirika kwako, Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi; |
16. | Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado. |
17. | Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake! |
18. | Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe. |
19. | Ee Mungu, laiti ungewafisha waovu! Enyi watu wa damu, ondokeni kwangu; |
20. | Kwa maana wakuasi kwa ubaya, Adui zako wakutaja jina lako bure. |
21. | Je! Bwana nisiwachukie wanaokuchukia? Nisikirihike nao wakuasio? |
22. | Nawachukia kwa ukomo wa chuki, Wamekuwa adui kwangu. |
23. | Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; |
24. | Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele. |
← Psalms (139/150) → |