← Psalms (138/150) → |
1. | Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi. |
2. | Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, Nitalishukuru jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako, Kwa maana umeikuza ahadi yako, Kuliko jina lako lote. |
3. | Siku ile niliyokuita uliniitikia, Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. |
4. | Ee Bwana, wafalme wote wa dunia watakushukuru, Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako. |
5. | Naam, wataziimba njia za Bwana, Kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu. |
6. | Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali. |
7. | Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa. |
8. | Bwana atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi za mikono yako. |
← Psalms (138/150) → |