| ← Psalms (136/150) → |
| 1. | Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 2. | Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 3. | Mshukuruni Bwana wa mabwana; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 4. | Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 5. | Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 6. | Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 7. | Yeye aliyefanya mianga mikubwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 8. | Jua litawale mchana; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 9. | Mwezi na nyota zitawale usiku; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 10. | Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 11. | Akawatoa Waisraeli katikati yao; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 12. | Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 13. | Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 14. | Akawavusha Israeli katikati yake; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 15. | Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 16. | Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 17. | Yeye aliyewapiga wafalme wakuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 18. | Akawaua wafalme mashuhuri; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 19. | Sihoni, mfalme wa Waamori; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 20. | Na Ogu, mfalme wa Bashani; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 21. | Akaitoa nchi yao iwe urithi; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 22. | Urithi wa Israeli mtumishi wake; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 23. | Aliyetukumbuka katika unyonge wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 24. | Akatuokoa na watesi wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 25. | Kila chenye mwili akipa chakula chake; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| 26. | Mshukuruni Mungu wa mbingu; Kwa maana fadhili zake ni za milele. |
| ← Psalms (136/150) → |