Psalms (13/150)  

1. Ee Bwana, hata lini utanisahau, hata milele? Hata lini utanificha uso wako?
2. Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?
3. Ee Bwana, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.
4. Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.
5. Nami nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.
6. Naam, nimwimbie Bwana, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

  Psalms (13/150)