← Psalms (128/150) → |
1. | Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake. |
2. | Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema. |
3. | Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Vyumbani mwa nyumba yako. Wanao kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako. |
4. | Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye Bwana. |
5. | Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako; |
6. | Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli. |
← Psalms (128/150) → |