← Psalms (126/150) → |
1. | Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, Tulikuwa kama waotao ndoto. |
2. | Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, Bwana amewatendea mambo makuu. |
3. | Bwana alitutendea mambo makuu, Tulikuwa tukifurahi. |
4. | Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa, Kama vijito vya Kusini. |
5. | Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha. |
6. | Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake. |
← Psalms (126/150) → |