Psalms (124/150)  

1. Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa,
2. Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Wanadamu walipotushambulia.
3. Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu
4. Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu;
5. Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu Maji yafurikayo.
6. Na ahimidiwe Bwana; Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao.
7. Nafsi yetu imeokoka kama ndege Katika mtego wa wawindaji, Mtego umevunjika, nasi tumeokoka.
8. Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.

  Psalms (124/150)