Psalms (123/150)  

1. Nimekuinulia macho yangu, Wewe uketiye mbinguni.
2. Kama vile macho ya watumishi Kwa mkono wa bwana zao Kama macho ya mjakazi Kwa mkono wa bibi yake; Hivyo macho yetu humwelekea Bwana, Mungu wetu, Hata atakapoturehemu.
3. Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu sisi, Kwa maana tumeshiba dharau.
4. Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha, Na dharau ya wenye kiburi.

  Psalms (123/150)