Psalms (122/150)  

1. Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana.
2. Miguu yetu imesimama Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.
3. Ee Yerusalemu uliyejengwa Kama mji ulioshikamana,
4. Huko ndiko walikopanda kabila, Kabila za Bwana; Ushuhuda kwa Israeli, Walishukuru jina la Bwana.
5. Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, Viti vya enzi vya mbari ya Daudi.
6. Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao;
7. Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.
8. Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe.
9. Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema.

  Psalms (122/150)