← Psalms (122/150) → |
1. | Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana. |
2. | Miguu yetu imesimama Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. |
3. | Ee Yerusalemu uliyejengwa Kama mji ulioshikamana, |
4. | Huko ndiko walikopanda kabila, Kabila za Bwana; Ushuhuda kwa Israeli, Walishukuru jina la Bwana. |
5. | Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, Viti vya enzi vya mbari ya Daudi. |
6. | Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao; |
7. | Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako. |
8. | Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe. |
9. | Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema. |
← Psalms (122/150) → |