| ← Psalms (121/150) → |
| 1. | Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi? |
| 2. | Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi. |
| 3. | Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye; |
| 4. | Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli. |
| 5. | Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume. |
| 6. | Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku. |
| 7. | Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako. |
| 8. | Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele. |
| ← Psalms (121/150) → |