| ← Psalms (120/150) → |
| 1. | Katika shida yangu nalimlilia Bwana Naye akaniitikia. |
| 2. | Ee Bwana, uiponye nafsi yangu Na midomo ya uongo na ulimi wa hila. |
| 3. | Akupe nini, akuzidishie nini, Ewe ulimi wenye hila? |
| 4. | Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, Pamoja na makaa ya mretemu. |
| 5. | Ole wangu mimi! Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki; Na kufanya maskani yangu Katikati ya hema za Kedari. |
| 6. | Nafsi yangu imekaa siku nyingi, Pamoja naye aichukiaye amani. |
| 7. | Mimi ni wa amani; Bali ninenapo, wao huelekea vita. |
| ← Psalms (120/150) → |