| ← Psalms (115/150) → |
| 1. | Ee Bwana, kutukuza usitutukuze sisi, Bali ulitukuze jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako, Kwa ajili ya uaminifu wako. |
| 2. | Kwa nini mataifa kusema, Yuko wapi Mungu wao? |
| 3. | Lakini Mungu wetu yuko mbinguni, Alitakalo lote amelitenda. |
| 4. | Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu. |
| 5. | Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni, |
| 6. | Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu, |
| 7. | Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake. |
| 8. | Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia. |
| 9. | Enyi Israeli, mtumainini Bwana; Yeye ni msaada wao na ngao yao. |
| 10. | Enyi mlango wa Haruni, mtumainini Bwana; Yeye ni msaada wao na ngao yao. |
| 11. | Enyi mmchao Bwana, mtumainini Bwana; Yeye ni msaada wao na ngao yao. |
| 12. | Bwana ametukumbuka, Naye atatubariki sisi. Ataubariki mlango wa Israeli, Ataubariki mlango wa Haruni, |
| 13. | Atawabariki wamchao Bwana, Wadogo kwa wakubwa. |
| 14. | Bwana na awaongeze ninyi, Ninyi na watoto wenu. |
| 15. | Na mbarikiwe ninyi na Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi. |
| 16. | Mbingu ni mbingu za Bwana, Bali nchi amewapa wanadamu. |
| 17. | Sio wafu wamsifuo Bwana, Wala wo wote washukao kwenye kimya; |
| 18. | Bali sisi tutamhimidi Bwana, Tangu leo na hata milele. |
| ← Psalms (115/150) → |