| ← Psalms (114/150) → |
| 1. | Haleluya. Israeli alipotoka Misri, Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni. |
| 2. | Yuda ilikuwa patakatifu pake, Israeli milki yake. |
| 3. | Bahari iliona ikakimbia, Yordani ilirudishwa nyuma. |
| 4. | Milima iliruka kama kondoo waume, Vilima kama wana-kondoo. |
| 5. | Ee bahari, una nini, ukimbie? Yordani, urudi nyuma? |
| 6. | Enyi milima, mruke kama kondoo waume? Enyi vilima, kama wana-kondoo? |
| 7. | Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana, Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo. |
| 8. | Augeuza mwamba kuwa ziwa la maji, Jiwe gumu kuwa chemchemi. |
| ← Psalms (114/150) → |