← Psalms (113/150) → |
1. | Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana. |
2. | Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele. |
3. | Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa. |
4. | Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu. |
5. | Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu; |
6. | Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani? |
7. | Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani. |
8. | Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake. |
9. | Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha. |
← Psalms (113/150) → |