← Psalms (112/150) → |
1. | Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake. |
2. | Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa. |
3. | Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele. |
4. | Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki. |
5. | Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki. |
6. | Kwa maana hataondoshwa kamwe; Mwenye haki atakumbukwa milele. |
7. | Hataogopa habari mbaya; Moyo wake u imara ukimtumaini Bwana. |
8. | Moyo wake umethibitika hataogopa, Hata awaone watesi wake wameshindwa. |
9. | Amekirimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu. |
10. | Asiye haki ataona na kusikitika, Atasaga meno yake na kuyeyuka, Tamaa ya wasio haki itapotea. |
← Psalms (112/150) → |