← Psalms (110/150) → |
1. | Neno la Bwana kwa Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwafanyapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako. |
2. | Bwana atainyosha toka Sayuni Fimbo ya nguvu zako. Uwe na enzi kati ya adui zako; |
3. | Watu wako wanajitoa kwa hiari, Siku ya uwezo wako; Kwa uzuri wa utakatifu, Tokea tumbo la asubuhi, Unao umande wa ujana wako. |
4. | Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki. |
5. | Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake. |
6. | Atahukumu kati ya mataifa, Ataijaza nchi mizoga; Ataseta kichwa katika nchi nyingi. |
7. | Atakunywa maji ya mto njiani; Kwa hiyo atakiinua kichwa chake. |
← Psalms (110/150) → |