| ← Psalms (108/150) → |
| 1. | Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, Nitaimba, nitaimba zaburi, Naam, kwa utukufu wangu. |
| 2. | Amka, kinanda na kinubi, Nitaamka alfajiri. |
| 3. | Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu, Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa. |
| 4. | Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni, Na uaminifu wako hata mawinguni. |
| 5. | Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako. |
| 6. | Ili wapenzi wako waopolewe, Uokoe kwa mkono wako wa kuume, uniitikie. |
| 7. | Mungu amenena kwa utakatifu wake, Nami nitashangilia. Nitaigawanya Shekemu, Nitalipima bonde la Sukothi. |
| 8. | Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu, Na Efraimu ni nguvu ya kichwa changu. Yuda ni fimbo yangu ya kifalme, |
| 9. | Moabu ni bakuli langu la kunawia. Nitamtupia Edomu kiatu changu, Na kumpigia Filisti kelele za vita. |
| 10. | Ni nani atakayenipeleka hata mji wenye boma? Ni nani atakayeniongoza hata Edomu? |
| 11. | Ee Mungu, si Wewe uliyetutupa? Wala, Ee Mungu, hutoki na majeshi yetu? |
| 12. | Utuletee msaada juu ya mtesi, Maana wokovu wa binadamu haufai. |
| 13. | Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu. |
| ← Psalms (108/150) → |