| ← Psalms (100/150) → |
| 1. | Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; |
| 2. | Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; |
| 3. | Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. |
| 4. | Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; |
| 5. | Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi. |
| ← Psalms (100/150) → |