Psalms (1/150)  

1. Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
2. Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
3. Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
4. Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5. Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
6. Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.

      Psalms (1/150)