| ← Lamentations (5/5) |
| 1. | Ee Bwana, kumbuka yaliyotupata; Utazame na kuiona aibu yetu. |
| 2. | Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni; Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri. |
| 3. | Tumekuwa yatima waliofiwa na baba; Mama zetu wamekuwa kama wajane. |
| 4. | Tumekunywa maji yetu kwa fedha; Kuni zetu twauziwa. |
| 5. | Watufuatiao wa juu ya shingo zetu; Tumechoka tusipate raha yo yote. |
| 6. | Tumewapa hao Wamisri mkono; Na Waashuri nao, ili tushibe chakula. |
| 7. | Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao. |
| 8. | Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao. |
| 9. | Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu; Kwa sababu ya upanga wa nyikani. |
| 10. | Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu; Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo. |
| 11. | Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni; Na mabikira katika miji ya Yuda. |
| 12. | Wakuu hutungikwa kwa mikono yao; Nyuso za wazee hazipewi heshima. |
| 13. | Vijana huyachukua mawe ya kusagia; Na watoto hujikwaa chini ya kuni. |
| 14. | Wazee wameacha kwenda langoni; Na vijana kwenda ngomani. |
| 15. | Furaha ya mioyo yetu imekoma; Machezo yetu yamegeuka maombolezo. |
| 16. | Taji ya kichwa chetu imeanguka; Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi. |
| 17. | Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia; Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema. |
| 18. | Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa, Mbweha hutembea juu yake. |
| 19. | Wewe, Bwana, unadumu milele; Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi. |
| 20. | Mbona watusahau sikuzote; Na kutuacha muda huu mwingi? |
| 21. | Ee Bwana, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale. |
| 22. | Isipokuwa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu. |
| ← Lamentations (5/5) |