← Job (5/42) → |
1. | Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu? Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu? |
2. | Kwani hasira humwua mtu mpumbavu, Nao wivu humwua mjinga. |
3. | Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake. |
4. | Watoto wake wako mbali na wokovu, Nao wamesongwa langoni, Wala hapana atakayewaponya. |
5. | Mavuno yake wale wenye njaa huyala, Na kuyatwaa hata kuyatoa miibani, Nao wenye kiu huzitwetea mali zao. |
6. | Kwani taabu haitoki mchangani, Wala mashaka hayachipuki katika nchi; |
7. | Lakini mwanadamu huzaliwa ili apate mashaka, Kama cheche za moto zirukavyo juu. |
8. | Lakini mimi ningemtafuta Mungu, Ningemwekea Mungu daawa yangu; |
9. | Yeye afanyaye mambo makuu, yasiyotambulikana; Mambo ya ajabu yasiyo na hesabu; |
10. | Yeye atoaye mvua inyeshe juu ya nchi, Na kuyapeleka maji mashambani; |
11. | Awainuaye juu hao walio chini; Na hao waombolezao hukuzwa wawe salama. |
12. | Yeye huyatangua mashauri ya wadanganyifu, Mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao. |
13. | Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao wenyewe; Na mashauri ya washupavu yaharibika kwa haraka. |
14. | Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, Hupapasa mchana vilevile kama usiku. |
15. | Lakini yeye huokoa na upanga wa kinywa chao, Hata kumwokoa mhitaji na mkono wake aliye hodari. |
16. | Basi hivi huyo maskini ana matumaini, Na uovu hufumba kinywa chake. |
17. | Tazama, yu heri mtu yule Mungu amwadhibuye; Kwa hiyo usidharau kurudiwa na huyo Mwenyezi. |
18. | Kwani yeye huumiza, lakini tena huuguza; Yeye hutia jeraha, na mikono yake huponya. |
19. | Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa. |
20. | Wakati wa njaa atakukomboa na mauti; Na vitani atakukomboa na nguvu za upanga. |
21. | Utafichwa na mapigo ya ulimi; Wala usiogope maangamizo yatakapokuja. |
22. | Wewe utayacheka maangamizo na njaa; Wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi. |
23. | Kwani utakuwa na mapatano na mawe ya bara; Nao wanyama wa bara watakuwa na amani kwako. |
24. | Nawe utajua ya kwamba hema yako ina salama; Na zizi lako utaliaua, wala usikose kitu. |
25. | Tena utajua ya kwamba uzao wako utakuwa mwingi, Na vizazi vyako watakuwa kama nyasi za nchi. |
26. | Utafika kaburini mwenye umri mtimilifu, Kama mganda wa ngano ulivyo wakati wake. |
27. | Tazama, haya tumeyapeleleza, ndivyo yalivyo; Yasikie, uyajue, ili upate mema. |
← Job (5/42) → |