← Job (29/42) → |
1. | Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema, |
2. | Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya kale, Kama katika siku hizo Mungu aliponilinda; |
3. | Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani, Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake; |
4. | Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa, Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu; |
5. | Wakati Mwenyezi alipokuwa akali pamoja nami, Nao watoto wangu walipokuwa wakinizunguka; |
6. | Wakati hatua zangu zilipokuwa zikioshwa kwa siagi, Nalo jabali liliponimiminia mito ya mafuta! |
7. | Wakati nilipotoka kwenda mjini, hata langoni, Nilipokitengeza kiti changu katika njia kuu, |
8. | Hao vijana waliniona wakajificha, Nao wazee wakaniondokea na kusimama; |
9. | Wakuu wakanyamaa wasinene, Na kuweka mikono yao vinywani mwao; |
10. | Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao. |
11. | Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia; Na jicho liliponiona, likanishuhudia. |
12. | Kwa sababu nalimwokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia. |
13. | Baraka yake yeye aliyekuwa karibu na kupotea ilinijia; Nikaufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha. |
14. | Nalijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba. |
15. | Nalikuwa macho kwa kipofu, Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea. |
16. | Nalikuwa baba kwa mhitaji, Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza. |
17. | Nami nilizivunja taya za wasio haki, Na kumpokonya mawindo katika meno yake. |
18. | Ndipo niliposema, Nitakufa ndani ya kioto changu, Nami nitaziongeza siku zangu kama mchanga; |
19. | Shina langu limeenea hata kufika majini, Na umande hukaa usiku kucha katika matawi yangu; |
20. | Utukufu wangu utakuwa mpya kwangu, Na uta wangu hurejezwa upya mkononi mwangu. |
21. | Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja, Wakanyamaa kimya wapate sikia mashauri yangu. |
22. | Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu; Matamko yangu yakadondoka juu yao. |
23. | Walikuwa wakiningojea kama kungojea mvua; Wakafunua vinywa vyao sana kama mvua ya masika. |
24. | Walipokata tamaa nikacheka nao; Na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha. |
25. | Niliwachagulia njia, nikakaa kama mkuu wao. Nikakaa kama mfalme katika jeshi la askari, Mfano wa awafarijiye hao waombolezao. |
← Job (29/42) → |