← Job (27/42) → |
1. | Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema, |
2. | Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu; Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu; |
3. | (Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani yangu, Na roho ya Mungu i katika pua yangu;) |
4. | Hakika midomo yangu haitanena yasiyo haki, Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu. |
5. | Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki; Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu. |
6. | Haki yangu naishika sana, wala sitaiacha; Moyo wangu hautanisuta wakati nikiwapo hai. |
7. | Adui yangu na awe kama huyo mwovu, Na mwenye kuondoka kinyume changu na awe kama asiye haki. |
8. | Kwani tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida, Hapo Mungu amwondoleapo roho yake? |
9. | Je! Mungu atakisikia kilio chake, Taabu zitakapomfikilia? |
10. | Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi, Na kumlingana Mungu nyakati zote? |
11. | Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu; Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha. |
12. | Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe; Mbona basi mmebatilika kabisa? |
13. | Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu, Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi. |
14. | Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga; Na wazao wake hawatashiba chakula. |
15. | Hao watakaosalia kwake watazikwa katika kufa, Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza. |
16. | Ajapokusanya fedha kama mavumbi, Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi; |
17. | Yumkini kuyatengeza, lakini wenye haki watayavaa, Nao wasio na hatia watazigawanya hizo fedha. |
18. | Yeye hujenga nyumba yake kama mdudu, Na kama kibanda afanyacho mlinzi. |
19. | Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho; Hufunua macho yake, naye hayuko. |
20. | Vitisho vyampata kama maji mengi; Dhoruba humwiba usiku. |
21. | Upepo wa mashariki humchukua, naye huondoka; Na kumkumba atoke mahali pake. |
22. | Kwani Mungu atamtupia asimhurumie; Angependa kuukimbia mkono wake. |
23. | Watu watampigia makofi, Na kumzomea atoke mahali pake. |
← Job (27/42) → |