| ← Job (26/42) → | 
| 1. | Ndipo Ayubu akajibu, na kusema, | 
| 2. | Jinsi ulivyomsaidia huyo asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono usio na nguvu! | 
| 3. | Jinsi ulivyomshauri huyo asiye na hekima! Na kutangaza ujuzi wa kweli kwa wingi! | 
| 4. | Je! Umetamka maneno kwa nani? Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako? | 
| 5. | Hao waliokufa watetema Chini ya maji na hao wayakaao. | 
| 6. | Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko. | 
| 7. | Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu. | 
| 8. | Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito; Na hilo wingu halipasuki chini yake. | 
| 9. | Husitiri uso wa kiti chake cha enzi, Na kulitandaza wingu lake juu yake. | 
| 10. | Amepiga duara kuwa ni mpaka juu ya uso wa maji, Hata hapo mwanga na giza vinapopakana. | 
| 11. | Nguzo za mbingu zatetemeka, Na kustaajabu kwa kukemea kwake. | 
| 12. | Huichafua bahari kwa uwezo wake, Na kumtema Rahabu kwa akili zake. | 
| 13. | Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake; Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio. | 
| 14. | Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake; Na jinsi yalivyo madogo manong'ono tusikiayo katika habari zake! Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuelewa nazo? | 
| ← Job (26/42) → |