| ← Job (25/42) → |
| 1. | Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema, |
| 2. | Enzi na hofu zi pamoja naye; Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka. |
| 3. | Je! Majeshi yake yahesabika? Ni nani asiyetokewa na mwanga wake? |
| 4. | Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu? Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke? |
| 5. | Tazama, hata mwezi hauangazi, Wala nyota si safi machoni pake; |
| 6. | Siuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu! |
| ← Job (25/42) → |