← Job (23/42) → |
1. | Ndipo Ayubu akajibu, na kusema, |
2. | Hata leo mashitaka yangu yana uchungu; Pigo langu ni zito zaidi ya kuugua kwangu. |
3. | Laiti ningejua mahali niwezapo kumwona, Nifike hata hapo anapokaa! |
4. | Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja. |
5. | Ningeyajua maneno atakayonijibu, Na kuelewa na hayo atakayoniambia. |
6. | Je! Angeshindana nami kwa ukuu wa uwezo wake? La, lakini angenisikiliza. |
7. | Hapo walekevu wangepata kuhojiana naye; Basi hivyo ningeachiliwa na mwamuzi wangu milele. |
8. | Tazama, naenda mbele, wala hayuko; Narudi nyuma, lakini siwezi kumwona; |
9. | Na mkono wa kushoto, afanyapo kazi, lakini siwezi kumwona; Hujificha upande wa kuume, hata nisimwone. |
10. | Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu. |
11. | Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka. |
12. | Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu, |
13. | Lakini yeye ni mmoja, ni nani awezaye kumgeuza? Tena nafsi yake ilitakalo, ndilo afanyalo. |
14. | Kwani yeye hulitimiliza hilo nililoamuriwa; Tena mambo mengi kama hayo ya pamoja naye. |
15. | Kwa hiyo naona taabu mbele ya uso wake; Nitakapofikiri, namwogopa. |
16. | Kwani Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia, Naye Mwenyezi amenitaabisha; |
17. | Maana sikufadhaishwa kwa sababu ya giza, Wala kwa sababu giza kuu limenifunika uso. |
← Job (23/42) → |