1Chronicles (8/29)  

1. Naye Benyamini akamzaa Bela, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Ashbeli, na wa tatu Ahiramu;
2. na wa nne Noha, na wa tano Rafa.
3. Na Bela alikuwa na wana; Adari, na Gera, na Abihudi;
4. na Abishua, na Naamani, na Ahoa;
5. na Gera, na Shufamu, na Huramu.
6. Na hawa ndio wana wa Ehudi. (Hao ndio wakuu wa mbari za baba zao miongoni mwa wenyeji wa Geba; nao wakawachukua mateka mpaka Manahathi;
7. na Naamani, na Ahoa, na Gera; aliwachukua mateka). Naye akamzaa Uza, na Ahihudi.
8. Na Shaharaimu akazaa watoto katika Bara-Moabu, baada ya kuwafukuza wakeze Hushimu na Baara.
9. Akazaliwa na Hodeshi, mkewe; Yobabu, na Sibia, na Mesha, na Malkamu;
10. na Yeusi, na Shakia, na Mirma. Hao ndio wanawe, wakuu wa mbari za baba zao.
11. Naye alikuwa amezaliwa na Hushimu, Abitubu, na Elpaali.
12. Na wana wa Elpaali; Eberi, na Mishamu, na Shemedi, ambaye ndiye aliyejenga Ono na Lodi, pamoja na vijiji vyake;
13. na Beria, na Shema, waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao miongoni mwa wenyeji wa Aiyaloni, wale ambao waliwakimbiza wenyeji wa Gathi.
14. Na Ahio, na Ghashaki, na Yeremothi;
15. na Zebadia, na Aradi, na Ederi;
16. na Mikaeli, na Ishpa, na Yoha; walikuwa wana wa Beria.
17. Na Zebadia, na Meshulamu, na Hizki, na Heberi;
18. na Ishmerai, na Izlia, na Yobabu; walikuwa wana wa Elpaali.
19. Na Yakimu, na Zikri, na Zabdi;
20. na Elienai, na Silethai, na Elieli;
21. na Adaya, na Beraya, na Shimrathi; walikuwa wana wa Shema.
22. Na Ishpani, na Eberi, na Elieli;
23. na Abdoni, na Zikri, na Hanani;
24. na Hanania, na Elamu, na Anthothiya;
25. na Ifdeya, na Penueli; walikuwa wana wa Shashaki.
26. Na Shamsherai, na Sheharia, na Athalia;
27. na Yaareshia, na Eliya, na Zikri; walikuwa wana wa Yerohamu.
28. Hao ndio waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao, katika vizazi vyao vyote, watu maarufu; na hao walikuwa wakikaa Yerusalemu.
29. Basi huko Gibea alikaa babaye Gibea, jina lake Yeieli, ambaye jina la mkewe aliitwa Maaka;
30. na mwanawe, mzaliwa wake wa kwanza, alikuwa Abdoni, na Suri, na Kishi, na Baali,
31. na Gedori, na Ahio, na Zekaria
32. Na Miklothi akamzaa Shimea. Na hao nao walikuwa wakikaa pamoja na ndugu zao huko Yerusalemu, kuwakabili ndugu zao.
33. Naye Neri akamzaa Kishi; na Kishi akamzaa Sauli; na Sauli akamzaa Yonathani, na Malkishua, na Abinadabu, na Eshbaali.
34. Na mwanawe Yonathani alikuwa Meribaali; na Meribaali akamzaa Mika.
35. Na wana wa Mika; Pithoni, na Meleki, na Tarea, na Ahazi.
36. Na Ahazi akamzaa Yara; na Yara akamzaa Alemethi, na Azmawethi, na Zimri; na Zimri akamzaa Mosa;
37. na Mosa akamzaa Binea; na mwanawe huyo alikuwa Refaya, na mwanawe huyo ni Ekasa, na mwanawe huyo ni Aseli;
38. naye Aseli alikuwa na wana sita, ambao majina yao ni haya; Azrikamu, na Bokeru, na Ishmaeli, na Shearia, na Obadia, na Hanani. Hao wote walikuwa wana wa Aseli.
39. Na wana wa Esheki nduguye ni hawa; mzaliwa wake wa kwanza, Ulamu, na wa pili Yeushi, na wa tatu Elifeleti.
40. Na wana wa Ulamu walikuwa watu hodari wa vita, wapiga upinde, nao walikuwa na wana wengi, na wana wa wana, watu mia na hamsini. Hao wote ndio waliokuwa wana wa Benyamini.

  1Chronicles (8/29)