← 1Chronicles (3/29) → |
1. | Basi hawa ndio wana wa Daudi, aliozaliwa huko Hebroni; Amnoni, mzaliwa wa kwanza, mwana wa Ahinoamu, Myezreeli; wa pili, Danieli, wa Abigaili, Mkarmeli; |
2. | wa tatu, Absalomu, mwana wa Maaka, binti Talmai, mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, mwana wa Hagithi; |
3. | wa tano, Shefatia, wa Abitali; wa sita, Ithreamu, kwa Egla, mkewe. |
4. | Sita alizaliwa huko Hebroni; na huko akamiliki miaka saba na miezi sita; na huko Yerusalemu akamiliki miaka thelathini na mitatu. |
5. | Na hawa alizaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani, wanne, wana wa Bathsheba, binti Eliamu; |
6. | na Ibhari, na Elishua, na Elipeleti; |
7. | na Noga, na Nefegi, na Yafia; |
8. | na Elishama, na Eliada, na Elifeleti, watu kenda. |
9. | Hao wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wana wa masuria; na Tamari alikuwa umbu lao. |
10. | Na mwanawe Sulemani alikuwa Rehoboamu; na mwanawe huyo alikuwa Abiya; na mwanawe huyo ni Asa; na mwanawe huyo ni Yehoshafati; |
11. | na mwanawe huyo ni Yehoramu; na mwanawe huyo ni Ahazia; na mwanawe huyo ni Yoashi; |
12. | na mwanawe huyo ni Amazia; na mwanawe huyo ni Uzia; na mwanawe huyo ni Yothamu; |
13. | na mwanawe huyo ni Ahazi; na mwanawe huyo ni Hezekia; na mwanawe huyo ni Manase; |
14. | na mwanawe huyo ni Amoni; na mwanawe huyo ni Yosia. |
15. | Na wana wa Yosia walikuwa hawa; Yohana mzaliwa wa kwanza, wa pili Yehoyakimu, wa tatu Sedekia, wa nne Shalumu. |
16. | Na wana wa Yehoyakimu ni hawa; mwanawe Yekonia, na mwanawe Sedekia. |
17. | Na wana wa Yekonia, huyo aliyechukuliwa mateka; mwanawe Shealtieli, |
18. | na Malkiramu, na Pedaya, na Shenazari, na Yekamia, na Hoshama, na Nedabia. |
19. | Na wana wa Pedaya; Zerubabeli, na Shimei; na wana wa Zerubabeli; Meshulamu na Hanania; na Shelomithi alikuwa umbu lao; |
20. | na Hashuba, na Oheli, na Berekia, na Hasadia, na Yushab-Hesedi, watu watano. |
21. | Na wana wa Hanania; Pelatia na Yeshaya; na wana wa Refaya, na wana wa Arnani, na wana wa Obadia, na wana wa Shekania. |
22. | Na wana wa Shekania ni hawa; Shemaya, na wana wa Shemaya; Hatushi, na Igali, na Baria, na Nearia, na Shafati, watu sita. |
23. | Na wana wa Nearia; Elioenai, na Hezekia, na Azrikamu, watu watatu. |
24. | Na wana wa Elioenai; Hodavia, na Eliashibu, na Pelaya, na Akubu, na Yohana, na Delaya, na Anani, watu saba. |
← 1Chronicles (3/29) → |