← 1Chronicles (25/29) → |
1. | Tena Daudi na maakida wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na matoazi; hii ndiyo hesabu ya wafanya kazi sawasawa na utumishi wao; |
2. | wa wana wa Asafu; Zakuri, na Yusufu, na Nethania, na Asharela, wana wa Asafu; walioamriwa na Asafu, aliyetabiri kwa amri ya mfalme. |
3. | Wa Yeduthuni; wana wa Yeduthuni; Gedalia, na Seri, na Yeshaya, na Hashabia, na Matithia, [na Shimei], watu sita; walioamriwa na baba yao Yeduthuni mwenye kinubi, aliyetabiri katika kumshukuru na kumsifu Bwana. |
4. | Wa Hemani; wana wa Hemani; Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, na Yeremothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, na Romanti-ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri, Mahaziothi; |
5. | hao wote ndio wana wa Hemani, mwonaji wa mfalme, kwa maneno ya Mungu, ili kuinua pembe. Naye Mungu akampa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu. |
6. | Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa Bwana, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme. |
7. | Na hesabu yao, pamoja na ndugu zao waliofundishwa kumwimbia Bwana, wote waliokuwa wastadi, walikuwa mia mbili na themanini na wanane. |
8. | Wakatupiwa kura ya ulinzi wao, sawasawa wote, mdogo kwa mkubwa, mwalimu kwa mwanafunzi. |
9. | Kura ya kwanza ikamtokea Yusufu, kwa Asafu; ya pili Gedalia; yeye na nduguze na wanawe, kumi na wawili; |
10. | ya tatu Zakuri, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
11. | ya nne Seri, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
12. | ya tano Nethania, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
13. | ya sita Bukia, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
14. | ya saba Asharela, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
15. | ya nane Yeshaya, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
16. | ya kenda Matania wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
17. | ya kumi Shimei, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
18. | ya kumi na moja Uzieli, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
19. | ya kumi na mbili Hashabia, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
20. | ya kumi na tatu Shebueli, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
21. | ya kumi na nne Matithia, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
22. | ya kumi na tano Yeremothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
23. | ya kumi na sita Hanania, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
24. | ya kumi na saba Yoshbekasha, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
25. | ya kumi na nane Hanani, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
26. | ya kumi na kenda Malothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
27. | ya ishirini Eliatha, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
28. | ya ishirini na moja Hothiri, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
29. | ya ishirini na mbili Gidalti, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
30. | ya ishirini na tatu Mahaziothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili; |
31. | ya ishirini na nne Romanti-ezeri, wanawe na nduguze, kumi na wawili. |
← 1Chronicles (25/29) → |