1Chronicles (25/29)  

1. Tena Daudi na maakida wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na matoazi; hii ndiyo hesabu ya wafanya kazi sawasawa na utumishi wao;
2. wa wana wa Asafu; Zakuri, na Yusufu, na Nethania, na Asharela, wana wa Asafu; walioamriwa na Asafu, aliyetabiri kwa amri ya mfalme.
3. Wa Yeduthuni; wana wa Yeduthuni; Gedalia, na Seri, na Yeshaya, na Hashabia, na Matithia, [na Shimei], watu sita; walioamriwa na baba yao Yeduthuni mwenye kinubi, aliyetabiri katika kumshukuru na kumsifu Bwana.
4. Wa Hemani; wana wa Hemani; Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, na Yeremothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, na Romanti-ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri, Mahaziothi;
5. hao wote ndio wana wa Hemani, mwonaji wa mfalme, kwa maneno ya Mungu, ili kuinua pembe. Naye Mungu akampa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu.
6. Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa Bwana, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme.
7. Na hesabu yao, pamoja na ndugu zao waliofundishwa kumwimbia Bwana, wote waliokuwa wastadi, walikuwa mia mbili na themanini na wanane.
8. Wakatupiwa kura ya ulinzi wao, sawasawa wote, mdogo kwa mkubwa, mwalimu kwa mwanafunzi.
9. Kura ya kwanza ikamtokea Yusufu, kwa Asafu; ya pili Gedalia; yeye na nduguze na wanawe, kumi na wawili;
10. ya tatu Zakuri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
11. ya nne Seri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
12. ya tano Nethania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
13. ya sita Bukia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
14. ya saba Asharela, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
15. ya nane Yeshaya, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
16. ya kenda Matania wanawe na nduguze, kumi na wawili;
17. ya kumi Shimei, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
18. ya kumi na moja Uzieli, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
19. ya kumi na mbili Hashabia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
20. ya kumi na tatu Shebueli, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
21. ya kumi na nne Matithia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
22. ya kumi na tano Yeremothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
23. ya kumi na sita Hanania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
24. ya kumi na saba Yoshbekasha, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
25. ya kumi na nane Hanani, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
26. ya kumi na kenda Malothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
27. ya ishirini Eliatha, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
28. ya ishirini na moja Hothiri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
29. ya ishirini na mbili Gidalti, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
30. ya ishirini na tatu Mahaziothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
31. ya ishirini na nne Romanti-ezeri, wanawe na nduguze, kumi na wawili.

  1Chronicles (25/29)